Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania

"Inaunganisha Tanzania na Dunia"
ISO Imethibitishwa 9001:2015; 14001:2015 & 45001:2018

Habari

SHILINGI BILIONI 73.5 KUJENGA MIUNDOMBINU YA KISASA KATIKA KIWANJA CHA NDEGE MTWARA.


image title here


SHILINGI BILIONI 73.5 KUJENGA  MIUNDOMBINU YA KISASA KATIKA KIWANJA  CHA NDEGE  MTWARA.

 
Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa amesema kuwa serikali inaendelea kuboresha  na kujenga viwanja vya ndege ili viwanja hivyo  viweze kutoa huduma za usiku na Mchana na viwe vya kisasa ,

Mbarawa ameyasema hayo  kwenya hafla ya utiaji Saini ya Mkataba wa usanifu na ujenzi wa jengo la Abiria, Vituo vya Zimamoto na Hali ya Hewa, Pamoja na Mnara wa kuongozea ndege katika kiwanja cha ndege cha Mtwara wenye thamani  ya shilingi bilioni 73.5.

“Serikali inaendelea kujenga na kuboresha viwanja vya ndege hapa nchini viwanja hivyo ni kiwanja  cha ndege cha Musoma, Iringa, Songwe , Msalato na kiwanja  cha ndege cha Mtwara ili viwanja hivyo viwe vya kisasa” Amesema Mbarawa.
 
Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya  Bunge ya Miundombinu Selemani Kakoso ameutaka uongozi wa wizara ya Uchukuzi kuhakikisha inamsimamia mkandarasi huyo ili akamailishe ujenzi huo kwa wakati .

“Kamati ya Bunge ya Miundombinu inaipongeza serikali kwa hatua hii, pia ni jambo jema kwa TAA kusimamia ujenzi huo kwani  umeweka vitu vyote vinavyohitajika hivyo Wizara hakikisheni mnamsimamia Mkandarasi ili akamilishe kazi hii kwa wakati, Alisema Kakoso.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Viwanja vya ndege  Tanzania Bw, Mussa Mbura amesema kuwa jengo hilo litakuwa na uwezo wa kuhudumia abiria milioni moja kwa  mwaka  na  500 kwa mara moja ikiwa mkataba huo utachukua miezi 36.

Mkataba huo umeingiwa na Serikali kupitia  Mamlaka ya viwanja vya ndege Tanzania (TAA) na kampuni ya China Railway Construction Engineering Group(CRCEG )kutoka nchi ya China.

 
Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa amesema kuwa serikali inaendelea kuboresha  na kujenga viwanja vya ndege ili viwanja hivyo  viweze kutoa huduma za usiku na Mchana na viwe vya kisasa ,

Mbarawa ameyasema hayo  kwenya hafla ya utiaji Saini ya Mkataba wa usanifu na ujenzi wa jengo la Abiria, Vituo vya Zimamoto na Hali ya Hewa, Pamoja na Mnara wa kuongozea ndege katika kiwanja cha ndege cha Mtwara wenye thamani  ya shilingi bilioni 73.5.

“Serikali inaendelea kujenga na kuboresha viwanja vya ndege hapa nchini viwanja hivyo ni kiwanja  cha ndege cha Musoma, Iringa, Songwe , Msalato na kiwanja  cha ndege cha Mtwara ili viwanja hivyo viwe vya kisasa” Amesema Mbarawa.
 
Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya  Bunge ya Miundombinu Selemani Kakoso ameutaka uongozi wa wizara ya Uchukuzi kuhakikisha inamsimamia mkandarasi huyo ili akamailishe ujenzi huo kwa wakati .

“Kamati ya Bunge ya Miundombinu inaipongeza serikali kwa hatua hii, pia ni jambo jema kwa TAA kusimamia ujenzi huo kwani  umeweka vitu vyote vinavyohitajika hivyo Wizara hakikisheni mnamsimamia Mkandarasi ili akamilishe kazi hii kwa wakati, Alisema Kakoso.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Viwanja vya ndege  Tanzania Bw, Mussa Mbura amesema kuwa jengo hilo litakuwa na uwezo wa kuhudumia abiria milioni moja kwa  mwaka  na  500 kwa mara moja ikiwa mkataba huo utachukua miezi 36.

Mkataba huo umeingiwa na Serikali kupitia  Mamlaka ya viwanja vya ndege Tanzania (TAA) na kampuni ya China Railway Construction Engineering Group(CRCEG )kutoka nchi ya China.