Kuhusu Usimamizi wa Mazingira wa Mamlaka
Mamlaka inaamini kuwa usimamizi mzuri wa mazingira ni muhimu kwa ukuaji na uendelevu wa Viwanja vya Ndege. Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) inatekeleza mipango ya mazingira ili kuhakikisha ukuaji endelevu wa viwanja vya ndege na kutimiza wajibu wa kijamii wa kutunza mazingira katika Viwanja vya Ndege.
Mpango wa Usimamizi wa Mazingira
Tunawajibika kwa upana wa mazingira katika viwanja vya ndege na kutoa kipaumbele kwa shughuli zinazoweza kuathiri mazingira. Lengo ni kuboresha ubora wa hewa ya ndani, kuboresha udhibiti wa taka, kupunguza kelele, kuongeza ufanisi wa matumizi ya nishati na kupunguza utoaji wa gesi chafu. Ili kufanikisha hili, TAA imetengeneza Sera ya Mazingira ambayo inalenga kuendesha na kuendeleza viwanja vya ndege kwa njia inayozingatia mazingira kwa kuongozwa na kanuni za ulinzi wa mazingira.
Sera ya Mazingira
Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) inathamini sana afya na ustawi wa wafanyakazi wake na wadau wengine wote wanaotumia na kutembelea viwanja vyake vya ndege na kila mtu ana haki ya kufanya kazi katika mazingira safi, salama na yenye afya. TAA inajitahidi mara kwa mara kupunguza athari mbaya za mazingira katika viwanja vya ndege. Shughuli katika viwanja vya ndege zinafanywa kwa njia inayofaa kimazingira na kanuni mbalimbali za ulinzi wa mazingira. Ili kufanikisha hili, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania imeweka kanuni zifuatazo za mazingira kwa vitendo:
Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania itaunganisha na kutumia Mfumo wa Usimamizi wa Mazingira (EMS) ndani la Mamlaka na kuendelea kuboresha utendaji wake katika mazingira.