Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania

"Inaunganisha Tanzania na Dunia"
ISO Imethibitishwa 9001:2015; 14001:2015 & 45001:2018

Dira, Dhima, Maadili Mkuu na Majukumu

DIRA

Kuwa mtoaji bora wa huduma za (uendeshaji) viwanja vya ndege duniani.

DHIMA

Kutoa huduma bora na uwezeshaji katika viwanja vya ndege kwa kuzingatia usalama na ufanisi kwa wadau wa Viwanja vya Ndege na nia ya kukuza uchumi na maendeleo ya jamii.

MAADILI MAKUU

Uadilifu

Ubunifu

Uwajibikaji

Kuwajali Wateja

Kufanya kazi kwa weledi

Kufanya kazi kwa pamoja

Ulinzi na Usalama Viwanjani

MAJUKUMU

1. Kusimamia, kuendesha, kuboresha na kuendeleza viwanja vya ndege vinavyomilikiwa na Serikali ya Tanzania Bara;

2. Kutoa huduma bora na salama katika kuwahudumia abiria, ndege na mizigo pale usafiri wa anga unapotumika ili kujenga taswira nzuri ya nchi kwa Mataifa mengine duniani;

3. Kutoa ushauri wa kiufundi kwa Serikali katika masuala yanayohusu uendelezaji wa viwanja vya ndege;

4. Kuhakikisha kwamba Sera za Serikali, Kanunina Taratibu zinazohusiana na masuala ya viwanja vya ndege yanatekelezwa kwa viwango vya kimataifa;

5. Kuishauri Serikali katika masuala ya kitaifa na kimataifa yanayohusu usimamiaji wa viwanja vya ndege pamoja na kanuni, ada na tozo zinazoendana na utoaji wa huduma hiyo;

6. Kuunga mkono maendeleo ya kitaifa na kiuchumi kwa kuhakikisha kuna kuwepo miundo mbinu na huduma muhimu.