Kiwanja cha Ndege Songwe
Historia fupi ya Kiwanja
Kiwanja cha ndege cha Songwe ni moja kati ya viwanja 59vinavyosimamiwa na kuendeshwa na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA). Kiwanja hiki kilianza shughuli za uendeshaji mwaka 2012baada ya kufungwa kwa kiwanja cha zamani na kukamilika kwa ujenzi wa miundombinu muhimu ya kiwanja hiki cha Songwe ikiwemo Jengo la abiria, Jengo la kuongozea ndege, Jengo la zimamoto, kituo cha utabiri wa hali ya hewa, barabara ya kutua na kurukia ndege, maegesho ya ndege, barabara ya kiungio na maegesho ya magari. Hapo kabla, huduma za ndege zilikuwa zikifanyika kiwanja cha Mbeya pale eneo la Mwanjelwa.
Kwa sasa kiwanja kinafanyiwa ukarabati na kinalenga kuhudumia ndege zenye uwezo wa kubeba abiria zaidi ya 200. Kwa hivi sasa kinahudumia ndege zenye uwezo wa kubeba abiria 70. Kiwanja kipo daraja 4D, ICAO Code HTGW, IATA code MBI. Zimamoto ni Daraja 6.
Viwanja vidogo vya Chunya na Mbeya
Kiwanja cha ndege cha Songwepia kinasimamia viwanja vidogo vilivyoko Mkoani Mbeya ambavyo viko chini ya Mamlaka ya Viwanja vya ndege Tanzania.
Kiwanja cha ndege Chunya.
Kiwanja hiki kilianzishwa enzi za Ukoloni miaka ya 1939 kikilenga kuhudumia ndege za walowezi wa mashamba ya Tumbaku na uchimbaji wa madini. Kiwanja hiki kina urefu wa mita 1,200 na upana wa mita 30. Kimejengwa kwa kiwango cha nyasi. Kina eneo lenye ukubwa wa Hekari 63.666, kwa sasa kiko kwenye mchakato ya kupata hati.
Kiwanja kidogo cha Ndege Mbeya
Kiwanja hiki pia ni kati ya viwanja vya zamani ambapo kwa sasa kimefungwa na eneo lake limebadilishiwa matumizi baada ya shughuli za usafiri wa anga kuhamishiwa Kiwanja cha ndege Songwe.
Miundombinu ya kiwanja
Kiwanja cha ndege Songwe kina barabara moja ya kutua na kurukia ndege ambazo ni Runway 09/27 yenye urefu wa mita 3334 na upana wa mita 60. Pia kuna eneo la maegesho ya ndege (Apron) lenye ukubwa wa mita 17,400 [194m X 89.9m]
Miundombinu na vifaa kwenye eneo la umma
Pia kuna huduma ya ATM, Mgahawa wa chakula, duka la vinywaji,maegesho ya magari
Huduma ya Zimamoto na Uokoaji
Kituo cha Zimamoto kipo kwenye daraja 6 kwa mujibu wa viwanja vya ICAO. Kina magari mawili ya kuzima moto.
Kina uwezo wa kuzima moto na kina magari 2,
Udhibiti wa ndege hai na Wanyama
Katika kuhakikisha usalama wa kiwanja unakuwepo wakati wote, kipo kitengo mahususi cha kukabiliana na wanyama,ndege hai na binadamu wanaoishi kuzunguka eneo la kiwanja.
Mashirika ya ndege yanayotoa huduma
Kiwanja kinatoa huduma kwa ndege zenye ratiba maalumu na zile zisizokuwa na ratiba maalumu (Adhoc). Hivi sasa tuna mashirika ya ndege ya ATCL na Precision Air.
Wateja wa pango
Miradi inayotekelezwa na TAA
katika mwaka huu wa fedha, Kiwanja cha Ndege cha Songwe kinaendelea kutekeleza Miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo ni pamoja na kufanya matengenezo ya Jengo la Zimamoto, Ujenzi wa Jengo la usalama kwa ajili ya kusimika mashine ya ukaguzi, Ukarabati wa mfumo wa umeme kutoka katika Jengo la jenereta, Ununuzi na Usimikaji wa matanki ya kuhifadhi maji, Ununuzi wa vifaa kinga vya Zimamoto na ununuzi wa vifaa vya mawasiliano. Miradi yote hii ipo katika hatua mbalimbali za Ununuzi.
Miradi inayotekelezwa na Serikali kupitia TANROADS
Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi - Sekta ya Ujenzi inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa Upanuzi na Ukarabati wa kiwanja cha Ndege cha Songwe ili kuboresha miundombinu iliyopo na hivyo kuwezesha ndege aina ya Boeing 787/Dreamlinner yenye uwezo wa kubeba abiria zaidi ya 200 kutumia kiwanja hiki.
Mradi huu upo katika hatua mbalimbali za utekelezaji kama ifuatavyo;